ورود به حساب

نام کاربری گذرواژه

گذرواژه را فراموش کردید؟ کلیک کنید

حساب کاربری ندارید؟ ساخت حساب

ساخت حساب کاربری

نام نام کاربری ایمیل شماره موبایل گذرواژه

برای ارتباط با ما می توانید از طریق شماره موبایل زیر از طریق تماس و پیامک با ما در ارتباط باشید


09117307688
09117179751

در صورت عدم پاسخ گویی از طریق پیامک با پشتیبان در ارتباط باشید

دسترسی نامحدود

برای کاربرانی که ثبت نام کرده اند

ضمانت بازگشت وجه

درصورت عدم همخوانی توضیحات با کتاب

پشتیبانی

از ساعت 7 صبح تا 10 شب

دانلود کتاب Imân na Uislam

دانلود کتاب ایمان و اسلام

Imân na Uislam

مشخصات کتاب

Imân na Uislam

ویرایش:  
نویسندگان:   
سری:  
 
ناشر: Hakikat Kitabevi Publications 
سال نشر: 2016 
تعداد صفحات: 112 
زبان: Swahili 
فرمت فایل : PDF (درصورت درخواست کاربر به PDF، EPUB یا AZW3 تبدیل می شود) 
حجم فایل: 657 کیلوبایت 

قیمت کتاب (تومان) : 48,000



ثبت امتیاز به این کتاب

میانگین امتیاز به این کتاب :
       تعداد امتیاز دهندگان : 8


در صورت تبدیل فایل کتاب Imân na Uislam به فرمت های PDF، EPUB، AZW3، MOBI و یا DJVU می توانید به پشتیبان اطلاع دهید تا فایل مورد نظر را تبدیل نمایند.

توجه داشته باشید کتاب ایمان و اسلام نسخه زبان اصلی می باشد و کتاب ترجمه شده به فارسی نمی باشد. وبسایت اینترنشنال لایبرری ارائه دهنده کتاب های زبان اصلی می باشد و هیچ گونه کتاب ترجمه شده یا نوشته شده به فارسی را ارائه نمی دهد.


توضیحاتی درمورد کتاب به خارجی



فهرست مطالب

DIBAJI
Tunanza kitabu na Basmala; jina lake Allah ndio lenye ulinzi bora
Zawadi zake hazina kipimo; Ni mwengi wa rehema na Anapenda
sana kuwaondolea waja madhambi na kuwasamehe.
Allahu ta’ala watu wote waliopo ardhini anawafungulia milango
ya kutafuta kile watakacho. Ameumba vitu venye faida na kuvituma
au kuteremsha kwa kila mtu. Na Anawaongoza nakupata furaha ya
kudumu. Na vile vile Anawaongoza Atakao kwenye njia sahihi
miongoni mwa wale watu ambao waliacha njia sahihi (siaratwalmustakim)
wakakufuru kwasababu ya kudanganywa na nafsi zao
potofu au makundi mabaya au vitabu vyenye madhara makubwa au
vyombo vya habari badae wakatubu. Na Anawaokoa kutoka
kwenye kuangamia kwa milele. Hawateremshie neema Zake wale
wenye jeuri ya kupindukia Anawaacha kuendelea kuishi ndani ya
upotofu wanaopenda na kuridhia. Siku ya mwisho(kiyama)
Atawasamehe wale Atakaopenda miongoni mwa waumini
watakaokuwa wanafaa kuingi moto(jahannam) na Atawaingiza
pepo(jana). Yeye pekee ndie muumbaji wakila kitu ambacho kina
uhai, Allah Ndiye Anayelinda kila kitu kwa mda wote dhidi ya hofu
na vitishio. Kwakujiamini wenyewe kwajina la Allahu ta’ala tukufu
nakutegemea msaada kutoka Kwake tunanza kuandika kitabu hiki.
Sifa njema ni zake Allahu ta’ala. Amani na baraka ziwe ju ya
kipenzi chake Mtume Muhammad alaihi-s-salam. Na sala bora
ziwendea watu wanyumba yake (Ahl al-Bayt) na juu ya wale wote
ambao wameipigania dini hi kusonga mbele(maswahaba zake/ as-
Sahabat al-kiram).
Maelfu ya vitabu vyenye thamani vimeandikwa kuhusu
mafundisho ya imani, yanayoamrishwa na yanayokatazwa na
uislamu, na vingi miongoni mwa vitabu hivi vimetafusiriwa kwenye
lugha tofauti tofauti za kigeni na kusambazwa kwa kila nchi. Kwa
upande mwengine, watu wabaya(zindiki) ambao hawaoni mbali na
– 5 –
majasusi waingereza mara kwa mara wanashambulia faida za
uislamu, ukarimu na mwanga wake yani yale yalioamrishwa na yale
yaliokatazwa kwamba haya yanakiuka na haki za binadamu na
kujaribu kuyafanyia mabadiliko pamoja na kudanganya waislamu.
Hata hivyo, ni shukurani kwamba sasa hivi kila sehemu (nchi)
wanavyuoni wakislamu wanafanya juhudi kubwa kueneza na
kuulinda Uislamu. Wanavyuoni waislamu kwa kusikia kutoka kwa
masahaba Mtume Sallallahu aleihi wa sallam watukufu walioandika
vitabu wanaitwa (Wanaviuoni wa Ahli-i sunnat). Hotuba sizizofaa
na makala kwa upande mwengine yameshuhudiwa ambayo
yanatajwa kuwa yametolewa kwa kutumia Kur’an na hadith za
mtume na kikundi cha watu ambao hawajapitia na kusoma vitabu
vilivyoandikwa na wanaviuoni wa Ahl ssuna. Hali yakuwa hotuba
hizi na makala haya yamethibishwa kuwa ye ufanisi usiofaa kwa
ndugu zetu waislamu, ila yanawonyesha tu ujinga wa mawakala
wake.
Mtu yeyote anayedai kuwa Muislam au akaonekana anasali
jamaa basi huyu mtu anafaa kutambulika kama Muislam. Badae
akionekana kwenye mazungumzzo yake kwa mfano, mandishi yake
au katika mwenendo wake ikitokea kitu ambacho kina hitilafu na
mafunzo ya iman kama yalivyoelezewa na wanavyuoni wa Ahl as-
Sunna, basi atambiwa kwamba anayoyafanya ni kinyume na
Uislamu na asipoacha yatamfanya kuwa mpotofu au murtadi(mtu
ambaye ametoka kwenye Uislamu baada yakua Muislamu). Na
atambiwa ku yaacha kabisa na kutuubu. Na kama kwakutumia akili
zake ndogo akapuuza yanayomwambiwa na kusema kwamba
hataacha anayoyafanya basi huyu anafahamika kuwa ni mpotofu au
murtadi. Hata akiendelea kusali sala (namaz) tanu kila siku, akaenda
Makka na akafanya hijja na akaendelea kufanya ibada tofauti na
kutenda mema hatoepuka janga hili hadi pale atakapoacha kufanya
mambo hayo yanayomfanya mtu kafir na akafanya toba[1] hatokuwa
Muislamu. Kwa kujifunza vizuri vitu ambavyo vinamfanya mtu
– 6 –
[1] Kufanya tauba ya madhambi maana yake ni kujuta kwakufanya
dhambi, kisha ukamuomba Allahu ta’ala msamaha, kwamfano,
kwakusema dua hi: “ Estaghfirullah al-adhim al-ladhi lailaha illa Anta
Huwal hayy-ul-qayyum wa atubu ilaih” na kumuahidi Allah kutorejea
kufanya madhambi tena.
kafiri, ni jukumu la kila Muislamu kujikinga mwenyewe dhidi ya
mambo yanayomtoa ndani ya Uislamu na kusababisha kuwa
murtadi, na pia anapaswa kutambua vyema makafiri na waongo
ambao wanajifanya kuwa Waislamu, hasa Majasus wauingereza na
kukaa mbali na madhara yao.
Rasulullah sall-Allahu ta’ala alaihi wa sallam alielezea katika
hadith-i-sherif kwamba habari za uongo na zenye makosa
zitatolewa ndani ya Kur’an al-karim na hadith-i-sherif
nakusababisha makundi sabini na mbili(72) potofu kujitokeza.
Hadith-i-sherif hi inafafanuliwa kwenye vitabu al-Beriqa na al-
Hadiqa, ambavyo vilinukuu hadith-i-sherif hi kutoka kwenye vitabu
viwill (2) maaruf Bukhari na Muslim. Hatupasui kuamini vitabu na
mihadhara ya kikundi hiki ambao wanajitokeza kwa majina kama
wanaviuoni wa kiislamu au profesa wa dini; na vilevile tunapasua
kuwa uangalifu ili tusianguke kwenye mitego ya wezi wa dini na
imani hawa. Zaidi ya hayo Waisilamu wasio nelimu au wenye elim
ndogo, makominisit, mafreemasons pamoja na mamisionari
wakikrisitu kwa upande mwengine maWahabi ambao wamepokea
mafunzo kutoka kwenye wangereza na mayahudi, wanafanya
jitihada kupoteza watoto wa Waisilamu kwa kufufua na kutumia
mbinu mpya. Wafanya wawezalo ili kuteketeza au Kuangamiza
Iman na Uislamu kwa kutumia makala yenye uongo, filamu, ukumbi
wa michezo, radio na matangazo ya runinga pia mitandao ya kijami
kama facebook, tweeter, whatsup, google, yahoo nakadhalika.
Wantumia mamilion ya fedha kufanikisha lengo hili. Wanaviuon
wakiislamu ‘rahimahumullah’ wamefanya jitihada kwa kuwajibu
watu hawo na wamendelea kuonyesha njia ya Allahu ta’ala ambayo
ni yenye furaha na uokovu. Miongoni mwa hao, tumechagua kitabu
kinachoitwa I’tiqad-nama kilichoandikwa na Mawlana Diya’ad-din
Khalid al-Bagdadi al-Uthmani ‘quddisa sirruh; ambaye nu
mwanachiuoni maarufu. I’tikad-nama ni kitabu kilichotafusiriwa
kwa lugha ya kituruki na marehem Haji Faizullah Efendi mkaazi wa
Kemah, Erzinjan, nakupewa jina Faraid al-fawaid na kuchapishwa
mwaka 1312 A.H Egypt. Tafsiiri hi imerahisishwa kwa jina Iman na
Uislamu. Toleo lake lakwanza ni mwaka 1966. Maelezo yetu
yamewekwa kwenye mabano ( ). Tunamshukur Allahu ta’ala kwa
Kutujaalia kuweza kuchapisha kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili na
– 7 –
kwa mara ya kwanza. Asili ya kitabu hiki I’tikad-nama, ni lugha ya
kifaaris na bado ipo kwenye maktab ya chuo cha Istanbul (Idara ya
Ibnul Emin Mahmud Kemak, nambari F. 2639). Tafsiir yake ya
Kituruki ilichapiswa na Hakikat Kitabevi) kwa jina la (Iman ve
Islam).
Katika kitabu (Durr-ul-muhtar) kilichoandikwa na mwanaciuoni
mukubwa Alauddin-i Haskefi “rahimahullahu ta’ala”, mwisho wa
mlango wa ndoa ya kafir anaelezea kwamba, “ binti wa kiislamu
alieolewa au kuposwa halafu akabalehe au kutimza miaka ya uzima
na akawa hajuyi nguzo za iman na hajitambui kama ni muislamu
basi ndoa yake inakuwa batili (anakuwa murtadi). Anapaswa
kufundishwa majina ya Allahu ta’ala na anafaa kuyarudia na
kusema na’amini haya. Kufafanuwa haya, mwanachouin Ibn Ab’d’n
rahmahullah ta’al alisema; mtoto wa kike anapokuwa mdogo,
hufuata itikadi ya wazazi wake; na anakuwa Muislamu. Lakini
anapokuwa (kubalehe) hafati tena itikadi ua wazazi wake
kwasababu anajamulia mwenyewe. Anapotimiza umri wa utu
uzima (kubalehe) na akawa hana elimu kuhusu Uislamu na
hajitambui kuwa Muislamu basi anakuwa murtadi. Akijifunza nguzo
sita za Iman bila kuamini na asipojua umuhimu wa Uislamu, basi
hata akitamka kalimatu tauhid (akitoa shahada) yani Lailaha illallah
Muhammad rasulullah hawezi kuendelea kama Muislamu. Anafaa
kufahamu mambo sita ndani ya (Amantu billah...) piaamri zake
Allahu ta’ala na Aliokataza kuyakubali na kuyatekeleza. Ibn Abidin
katika uchambuzi hu anaonyesha kwamba mtu kafir akisema
kalimatu ttauhid na akamini maana yake basi mda huo anakuwa
Muislamu. Lakini kama waislamu wengine akipata nafasi anafaa
kukariri maneno yafatayo pamoja na maana yake: “Amantu bi’llahi
wa Mala’ikatihi wa Kutubihi wa Rusulihi wal-yawm-il-akhiri wa
bil-qadari khairihi wa sharrihi minallahi ta’ala walba’thu ba’dal
maut haqqun ash-hadu an la ilaha illallah wa ash-hadu anna
Muhammadan abduhu wa Rasuluhu.” Pia mtoto wa kiume (kijana)
ambaye ni Muislamu asipojifunza nguzo sita hizi na akasema
kwamba anazamini anakuwa murtadi anapofikisha umri wa watu
wazima( kubalehe). Bada ya kujifunza nguzo hizi sita na kuzamini
basi anakuwa amepata imani, bada ya hapo anawajibika kutafuta
mafundisho ya kiislamu yote na kujielimisha, kwa mfano kujua amri
– 8 –
za Uislamu zinazoitwa farz na yaliokatazwa yanayoitwa haramu,
jinsi ya kutia udhu, kuoga, sala inasiliwa vipi, mtu anasitiri vipi
(awrat) utupu wake/sehemu za siri. Anapouliza mtu kuhusu
mafunzo haya basi ni lazima kwa yule alieuilwa kumfundisha au
kumuelekeze kitabu sahihi kitakachomsaidia kupata maelezo hayo.
Akikosa kupata kitabu au mwalimu basi ni lazima atafute mmoja au
kitabu. Binti wa kike muislamu naye anawajibika kama
anavyowajibika mtoto wa kiume. Basi pale anaposhindwa kutafuta
mwalimu au kitabu kuhusu dini yake ya Uislamu anakuwa kafir.
Atapata udhuru kwakutojua endapo atendelea kutafuta mwalimu
au kitabu sahihi kya kiislamu asipotafuta basi anakuwa kafir moja
kwa moja. Muislamu ambaye hatimizi farz (yale yalioamrishwa na
Uislamu) kwa wakati wake au akatenda maovu(haramu) basi
ataingizwa kenye moto jahanam. Kitabu hiki kya Iman na Uislamu
kinaelezea kwa kina mafunzo kuhusu nguzo sita za iman. Basi kila
Muislamu anapaswa kusoma kitabu hiki vizuri na afanye awezalo ili
watoto wake na wale anowajua wapate kukisoma. Sehemu za
awrat (utupu) zimefafanuliwa zaidi katika kitabu Endless Bliss juzu
ya nne. Katika mandishi ya kitabu kiki maana ya ayet-i kerimas
imeitwa ma’al inayomanisha ‘maana kama yalivyotolewa na
wanaviuoni wa Tasfiir; kwani ayet-i karima au Kur’an maana yake
aliifahamu Mtume Sall-Allahu alaihi wasala peke yake ; na halafu
aliwafundisha masahaba zake. Wanaviuon wa tafsiir (ufafanuzi wa
Qur’an al-karim) walitofautisha na kuchuja hadith zilizoletwa na
wanafik na mazindiki ambao walipata mafunzo ya dini kutoka kwa
Waingereza kama watu wasiofuata madhehebu ili waweze
kuiharibu dini, na kuhusu zile hadith sherif wasizofahamu
wanazitafsiir kulingana na maoni yao. Kinachofahamika na watu
hao ambao hawajasoma dini ya Uislamu na wanasema kiarabu bila
ilimu ya Tafsiir, basi ufafanuzi wao haujulikani kama tafsiir ya
Qur’an tukuf. Ndio sababu hadith-i sherif inasema kwamba: ‘Mtu
anayetafsir Qur’an karim(tukufu) kulingana na ufahamu wake
basi anakuwa kafir.’ Kamusi ya kiarabu na maneno mengine
yasiokuwa ya kingereza na ni mageni kwa msomaji wa kingereza
yanaongezwa.
Tunamuomba Allahu ta’ala Atuongoze kwenye njia sahihi
ambayo ilionyeshwa na maulamaa wa Ahl as-Sunna! Tunamuomba
– 9 –
pia Atulinde dhidi ya kuamini uongo, udanganyifu na kuendelea
kukubali uongo wa madui wa Uislamu wanaojiita la-madhab yani
wasiokuwa na madhabu rasmi wanaotumia majina kama ‘
maulamaa wakuu wa Uislamu’!
Vitabu vyote vinavyochapishwa kwenye lugha nyingi tofauti
vinasambazwa ulimwengu kote kwa kutumia mtandao wa internet.
KUMBUSHO: wa kristu wanajitahidi kuutangaza ukrisitu,
Wayahudi nao wanajaribu kueneza Talmud, Hakikat Kitabevi
wanafanya wawezalo kutangaza Uislamu na wa freemasons
wanapigania kuhangamiza dini. Mtu mwenye akili, mwenye elimu
na mwenye hoja atatumia mantik yake na kufanya chaguo sahih.
Kwakutoa msada kwa kuenezaji wa njia sahih, itakuwa sabubu ya
binadamu kupata furaha katika dunia hi na badae(Akhira).
Ulimwengu wa Uislamu hivi sasa umegawanyika kwenye
makundi makuu matatu. Kundi la kwanza ni Waislamu wa ukweli
ambao wanafuata nyayo za ma Sahaba wa Mtume Sallallahu wa
sallama. Na hao wanaitwa Ahl as-Sunna au Sunni Muslims au
Firqa-i-naajiya, inayomanisha kundi ambalo limejiokoa kwenye
moto. Kundi la pila ni madui wa masahaba, na hao wanaitwa Shi’i (
mashia) au Firqa-i-dalla (kundi lililopotea) . kundi la tatu linaitwa
Wahhabi au Najid, mahali pa kuzaliwa kwao ni Najid Uarabuni. Na
vilevile wanajulikana kama Firqa-i-mal’uuna (kundi lililola’niwa). Na
katika kitabu chetu kinachoitwa Endless Bliss (Neema zisizo na
mwisho) na The Rising and the Hereafter (Kufufuka na Kiyama)
inaelezewa kwamba watu hawa wanaita Waislamu ‘makafir’. Na
Mtume wetu Sallallahu aleih wasallama alilaani watu wanoita
Waislamu vile. Uislamu kugawanyika kwenye makundi matatu haya
ni natija/matokeo ya hila za Wayahudi na Waingereza.
Kila Muislamu anapaswa kusema “La ilaha il-l-Allah,” mda wote
ili kuitukuza nafsi yake, mfano kuitukuza nafsi yake kutokana na
ujinga na maovu ambayo yanarithiwa na maumbile, na daima
anafaa kurudia dua hi “Estaghfirullah,” ili autakase muoyo wake,
mfano kuokoa moyo wake kutokana na ukafir na maovu ambayo
yamefunika moyo wake kwa sababu ya nafsi yake kujingiza kwenya
kundi la shetani na maovu, na katika kusoma vitabu hatari. Dua za
watu wenye kuufuata Uislamu na kufanya tawba kwa makosa yao
– 10 –
waliofanya watakubaliwa na Allahu ta’ala. Mtu asiposali
namazi(sala) tano kila siku, na akawatizama wanawake ambao
hawajajifunika vizuri na wengine wanaonesha awrat( utupu) wao,
na akala akanywa yale yalio haramu kula na kunywa, basi
itahitimishwa kwamba mtu huyu hafuati Uislamu. Na dua zake
hazitokubalika.
Miladi Hijri Shamsi Hijri kamari
2001 1380 1422




نظرات کاربران